• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WAHIMIZWA KUJENGA VYOO BORA

Posted on: February 23rd, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo jana amefanya ziara katika kijiji cha Lositete. Katika ziara hiyo aliambatana na watendaji wa Wilaya, na alifanya mkutano wa hadhara na wananchi na kusikiliza changamoto zao mbalimbali.

 Katika mkutano wake na wananchi wa kijiji cha Lositete Mhe. Theresia  amehimiza wananchi kujenga vyoo bora. Kauli mbiu ya uhamasishaji wa ujenzi wa maliwato ni, NYUMBA NI CHOO. Amesema vyoo vingi ni vya kienyeji havijaezekwa vizuri, havina mlango na havijazibwa kwa juu. Tukijenga vyoo vizuri tutajiepusha na magonjwa ya mlipuko yanayoletwa kutokana na ukosefu wa vyoo na kutozingatia usafi wa afya zetu.

Mhe. Theresia amesema maradhi ni adui namba moja, amesema jinsi tunavyojenga nyumba bora tujenge na vyoo bora pia. Amesema wananchi tujali afya zetu, na tuzingatie yale tuliyoambiwa na wataalamu. Mhe. Theresia amegusia swala la ujenzi wa hospital ya wilaya ambayo kwa sasa msingi wa jengo la utawala na msingi wa jengo la wagonjwa wa nje umekamilika. Ameomba wananchi kujitolea kujenga hospitali ya wilaya, ili iweze kukamilika haraka.

Bibi Afya Sauda Leveri amesema choo bora kina ukuta wa matofali na lazima kiwe na mlango na uwe na kitasa ndani kwa sababu ya usiri. Choo cha asili kina shimo kwenda chini na sakafu ya udongo, ukuta wake unaweza kuwa wa miti uliokandikwa kwa udongo na  mlango lakini pia huezekwa kwa paa au nyasi. Choo kilichoboreshwa kina bomba nje la kutolea hewa chafu, na inzi akiingia hawezi kutoka na hata akitoka anakufa. Choo cha maji kina sinki na kinatumia maji kuondoa uchafu, ( Smart latrine ) Choo chenye sinki kina kizibo kinachoziba tundu.

Awali katika taarifa yao iliyosomwa na ndugu Jakson Tango mwenyekiti wa kijiji cha Lositete amesema  kitongoji cha Lengitima kina kaya zenye vyoo bora tano, na kaya zenye vyoo vya asili ni mia moja kumi na tatu. kitongoji cha Kituma  kina kaya mbili  zenye vyoo bora na kaya mia hamsini na tisa  zina  vyoo vya asili. Kitongoji cha Selela kina kaya moja yenye choo bora na kaya mia kumi na tisa zina vyoo vya asili.

Mwenyekiti  ndugu Jakson amesema ofisi ya kijiji imefanya uhamasishaji kwa kutoa elimu na msako kwa kaya zisizo na choo. Amesema licha ya uhamasishaji huo bado kuna baadhi ya watu hawatumii  maliwato. Kabla ya elimu ya uhamasishaji kutolewa kulikuwa na kaya mia na ishirini zilizokuwa hazina vyoo kabisa na kaya mia mbili sabini na moja zilikuwa na vyoo vya asili. Mwenyekiti ndugu jakson amesema kaya nane pekee ndizo zilikuwa na vyoo bora, amesema changamoto nyingine ni wananchi wengi kutoweka na kutumia vyombo vya kunawia mikono baada ya kutoka maliwatoni.

 

Bibi, Afya Sauda Leveri akieleza kwa vitendo jinsi ya kujenga choo bora.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa