• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WANAVIKUNDI WAKABIDHIWA MASHINE, KUTENGENEZA NISHATI MBADALA

Posted on: December 6th, 2019

Shirika la United Nations Development Programs (UNDP) kwa kushirikiana na wataalamu wa chuo kikuu cha SUA wamekabididhi mashine kumi za kutengenezea nishati mbadala ya kutumia masalia ya shambani. Makabidhiano yamefanyika mbele ya ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Karatu.

Mgeni rasmi katika Makabidhiano hayo ya vifaa na mashine ni Mkuu wa wilaya ya karatu, ambaye aliwakilishwa na Ndugu Lameck Karanga Katibu Tarafa wa karatu.  Ndugu Lameck amesema mashine hizo kumi ambazo zimegawiwa kwa vikundi kumi  ni jitihada za kukabiliana na uharibifu wa mazingira. Ndugu Lameck ametoa salamu za shukrani na pongezi kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo. Ndugu Lameck amesema tukio hilo ni tukio muhimu na rafiki kwa jamii yetu inayopakana na hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni kivutio na kitega uchumi kwa taifa la Tanzania, amesema mradi huu wa kukabiliana na  uharibifu wa mazingira utakuwa endelevu. Mradi huu utaifanya Karatu kuwa ya kijani kwa kuepukana na kukata miti hovyo. Ndugu  Lameck amepongeza wataalamu kutoka SUA ambao wamesaidiana na shirika la UNDP amesema watendaji na wananchi wa Karatu ni waadilifu, watatunza   mashine na matokeo mazuri ya matumizi ya nishati mbadala yataonekana.

NDUGU LAMECK KARANGA AKIKABIDHI MASHINE KWA WANAKIKUNDI KWA NIABA YA MKUU WA WILAYA YA KARATU

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Ndugu Godfrey Luguma, ameshukuru shirika la UNDP kwa msaaada wa vifaa hivyo kwa wanavikundi. Ameahidi kutumia wanavikundi kuongeza ufahamu wa kujifunza zaidi kuhusu nishati hiyo mbadala ambayo ni mkombozi kwa wananchi lakini pia kujenga  fursa ya kiuchumi  kwa kuzalisha nishati hiyo na kuiuza.

Naye Mhadhiri wa chuo kikuu cha sua Dkt. Nikson Peter Mkiramweni akisoma taarifa yake amesema mradi ulianza mwaka jana na kuzinduliwa rasmi 1/10/2018. Mradi uliandikwa na wanataaluma wa SUA, baada ya kukithiri kwa tatizo la kukata miti kwa ajili ya mkaa kwenye hifadhi ya Ngorongoro. Dkt, Nikson amesema waliamua kulipunguza hilo tatizo kwa kuleta nishati mbadala kwa kutumia masalia ya mbaazi, maganda ya karanga, vifuu vya nazi, maranda ya mbao lakini pia magunzi. Amesema lengo la mradi ni kuwajengea uwezo wanajamii na kutengeneza nishati mbadala na kuuza. Amesema wamefanya mafunzo kwenye vijiji ilikuwajengea uwezo wananchi katika vijiji na kuwapa mafunzo ya ujasirimali kwa vikundi. Amesema vikundi viliundwa kwa hiari, katika kujikita katika kuleta faida kwa wanakikundi, amesema wao kama wataalamu walifanya utafiti kuhusu soko la nishati hiyo na kugundua uhitaji wa soko kwa ajili matumizi ya nishati hiyo mbadala upo.

Dkt.Niksoni amesema mkaa huo mbadala unatumika kidogo kwa matumizi makubwa kulinganisha na mkaa wa kawaida kwa sababu unaungua kidogo kidogo. Amesema mkaa huo hauna moshi unaoumiza macho, amesema vifaa vilivyonunuliwa vimekabidhiwa kwa Halmashauri ya wilaya ili vikabidhiwe kwa wanavikundi.

Mmoja wa wanakikundi aliyekabidhiwa Mashine kutoka kikundi cha kilimamoja ndugu Faustini Bura amesema mashine hizo zitasaidia kuepusha uharibifuwa misitu kwa sababau mashine inatumia masalia ya mazao ili kutengeneza nishati ya mkaa. Tofauti na hapo awali uzalishaji wa mkaa kwa bishara na matumizi ya nyumbani ulitegemea kukata miti. Amesema mradi huo utawasaidia kiuchumi watafanya biashara ya mkaa mbadala ili kujitengenezea kipato.

MAPIPA YA KUCHOMEA NISHATI NA MASHINE KATIKATI VIKIWA VIMEPANGWA PAMOJA.

WANAKIKUNDI NA WATAALAM WAKISHIRIKIANA KUCHOMA KWA KUTUMIA PIPA LIKIWA MASALIA YA MBAAZI TAYARI KUTENGENEZA MKAA KAMA INAVYOONEKANA.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa