• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WANAWAKE WAHAMASISHWA KUTAMBUA FURSA ZA UCHUMI

Posted on: March 8th, 2021

Wanawake ni watu muhimu katika kukuza uchumi wa nchi na uchumi wa familia. Tunatakiwa tuendelee kupambana ili tuweze kutengeneza mazingira mazuri ya uchumi ili tuweze kuimarika kiuchumi na tuweze kusomesha watoto wetu na kushiriki katika  ujasiriamali na vikundi vya  vikoba.

Hayo yamesemwa na Bi, Faraja Msingwa Katibu tawala wa wilaya ya Karatu aliyemwakilisha  Mkuu wa wilaya ya Karatu Katika kilele cha sherehe ya siku ya wanawake kilichofanyika katika uwanja wa Mazingira Bora Karatu. Kauli mbiu ya sherehe ya siku ya mwanamke ni mwanamke katika uongozi: chachu ya kufikia dunia yenye usawa.

Bi,  Msigwa amehimiza wanawake kushiriki katika vikoba na saccos ikiwa ni pamoja na kujihusisha na ujasiriamali ili waweza kupata fursa ya mikopo inayotolewa na Halmashauri. Amesema idara ya maendeleo ya jamii inapaswa kuja na mkakati wa kutoa elimu ya Ujasiriamali kwa wanawake ili waweze kutambua fursa za uchumi zinazopatikana  katika maeneo wanayoishi.

Bi Msigwa amesema serikali imeendelea kuthamini juhudi za maendeleo zinazofanywa na wanawake,  hivi sasa serikali imeongeza jina la mwanamke katika hati kumiliki ardhi ili kujenga mazingira ya usawa katika haki ya kumiliki ardhi. Katika uongozi serikali bado imeendelea kujenga usawa wa kijinsia, kwa kuongeza nafasi za viongozi wanawake, ameongeza kusema wanawake wanapaswa kujitokeza kugombea na kushindana sera pindi fursa za uongozi zinapotangazwa.

 Akizungumzia kuhusu mikopo Bi, Msigwa amesema lazima kuwe na nidhamu ya kukopa mikopo kwenye vikundi, amesema wanawake  wamekuwa na tabia ambayo si nzuri ya watu kuchukua fedha za mikopo na kufanya shughuli ambazo hazisaidii kumjengea uwezo mkopaji kurudisha fedha kwa wakati. Amesema ni vyema wanawake watambue umuhimu wakujishughulisha katika shughuli za maendeleo ili mikopo iweze kusaidia kuimarisha shughuli za uzalishaji.

Katibu tawala wa wilaya ya Karatu Bi, Faraja Msigwa (katikati)  pamoja Na Mwenyekiti wa Halmashauri  Mh. Lucian wakiwa  wameshikilia check tayari kwa kukabidhi vikundi 96 vya wakinamama vijana na walemavu.

Awali katika risala yao wanawake wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu iliyosomwa na Bi, Honoratha Sulle amesema vitendo vya ukatili wa kijinsia vinawaelemea zaidi wanawake na watoto. Amesema jamii, vyama vya siasa vinapaswa kuwa na mtizamo chanya juu ya maendeleo ya wanawake, ikiwa ni pamoja na kurekebisha mila na desturi zinazowabagua wanawake.

Amesema jamii  inapaswa ihamasishe kwa ujumla juu ya umuhimu wa utekelezaji shughuli mbalimbali za serikali kwa malengo ya kudumisha amani na upendo. Amesema hiyo itasaidia kujenga mshikamano kwa wanawake wote ambao utawekewa msisitizo katika kauli mbiu za siku ya mwanamke ili kujenga umoja. Amesema utaratibu wa kukemea mfumo dume uliopo imesaidia kupunguza adha wanazokumbana nazo wanawake katika maisha ya kila siku.

Bi, Sulle amesema lazima wanawake wahamasishwe kupeleka vijana wao wa kike shule, huku wakiendelea kupewa elimu ya jinsia na maendeleo kwa malengo ya kung’amua fursa za uchumi walizonazo katika mazingira yanayowazunguka ikiwa ni pamoja na kuwapa ujuzi.

Matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake katika uwanja wa mazingira Bora

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa