• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WANUFAIKA WA TASAF KARATU WAISHUKURU SERIKALI KWA FEDHA ZA RUZUKU

Posted on: November 7th, 2024

Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya Masikini halmasahuri ya Karatu, mradi unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii -TASAF, wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya awamu ya sita kwa kuwapatia fedha za ruzuku ya mpango huo.

Wamesema kuwa fedha hizo zimewasaidia kumudu kupata mahitaji ya nyumbani ya familia, mahitaji ya watoto wa shule pamoja na kupata elimu ya ujasiriamali ya kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa fedha ambazo zimewapa mitaji ya kuanzisha miradi ya biashara ikiwemo kilimo na ufagaji.

Eladia Saruwat mkazi wa Rhotia, amekiri kunufaika na fedha hizo za ruzuku na zimemsaidia kukidhi mahitaji ya familia sambamba na kuwawezesha watoto wake kwenda shule wakiwa na mahitaji muhimu ya shule.

"Tunamshukuru rais wetu mama Samia, TASAF imetupa elimu ya ujasiriamali, tumeanzisha vikundi vya kuweka na kukopa, fedha ambazo zimetusaidia kupata mitaji na kuanzisha biashara ndogondogo" .Amesema Agatha.

Naye Marjat Kimolo amesema kuwa, TASAF imewawezesha kukuza mitaji yao kwenye kilimo na ufugaji, jambo ambalo limekuza uchumi wa kaya zao.

Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF imetoa ruzuku ya shilingi milioni 134.6 kwa kaya 5,451 kwenye vijiji 61 vya Halmashauri hiyo ya Karatu ikiwa ni ruzuku ya mwezi Julai na Agosti, kwa mwaka wa fedha 2024/2025

Kaimu Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Karatu Ndg. Atanas Sarwath, amekiri kupokea fedha hizo na tayari zoezi la malipo kwa kaya zilizo kwenye Mpango limeanza tarehe Novemba 04,2024 na litakamilika Novemba 10,2024.

"Tumepokea shilingi 134.6 kwa ajili ya kaya 5,451 ambapo kwa ajili ya ruzuku ya elimu na afya ambapo shilingi milioni 91.8 zitalipwa kwa fedha taslimu na Milioni 42. walengwa watalipwa kwa njia ya benki na mitandao ya simu".Amefafanua Kaimu Mratibu huyo.


Ameongeza kuwa fedha hizo zinawasaidi walengwa katika kujikimu na mahitaji ya familia ikiwemo chakula mahitaji ya shule kwa watoto, pamoja na kupata mitaji ya kuanzisha biashara ndogongo huku kaya zikiunda vikundi vya kuwekeza fedha na kukopeshana.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa