• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WASIMAMIZI WA ICHF: WAWEKWA SAWA KUANZA KAZI

Posted on: June 21st, 2019

Wasimamizi watakao husika na mfumo wa usajili ICHF wamefanya semina ya siku mbili katika ukumbi wa Halmashauri. Semina hiyo imelenga kuwapa uwezo wa kufahamu mambo yanayohusu mfumo wa usajili wa ICHF iliyoboreshwa pamoja na kujifunza namna ya kutumia mfumo wa usajili.

Ndugu Emmanuel Carl muwezeshaji wa semina hiyo kwa wasimamizi (incharge) anasema, ICHF iliyoboreshwa inamwezesha mwananchi kupata matibabu kwa gharama nafuu. Semina hiyo ya ufahamu itasaidia wasimamizi hao kuhamasisha wananchi katika maeneo yao. Semina hiyo imetumika kuwawekea mfumo wa kutumia kwa njia ya simu ili kusajili watu katika ICHF. Pamoja na kuelekezwa namna za kutumia mfumo huo kwa ufasha ukihusisha Maafisa Tehama katika kutoa elimu.

Dkt Vicent Gyunda akitoa nasaha kwa wasimamizi 


Ndugu Emmanuel amesema uhamasishaji ni vyema ukafanyika katika vikao vya kijiji, kata na Tarafa. Amesema kuna uhusiano mkubwa kati ya msimamizi wa ICHF na kituo kupata fedha nyingi kwa sababu ya uhamasishaji ya watu kutumia ICHF. Amesema ni lazima huduma iwe nzuri wakati wa mapokezi kwa wateja wa ICHF na sehemu ya dawa. Amesema utaratibu wa kutumia bima ya afya unaanza kwa kupata huduma zahanati na kama tatizo la ugonjwa nia kubwa  unapewa hati kwenda kituo cha afya. Lakini kwa mteja aliyejiandikisha na ICHF aliyepata dharura mbali na eneo lake la makazi anaweza kupata matibabu katika kituo cha afya kilichopo karibu naye.

Ndugu Emammanuel amesema lengo ni kuwawezesha wananchi kutumia ICHF iliyoboreshwa na kuachana na mfumo wa kutoa malipo ya hapo kwa hapo. Upo muswada utakao  pelekwa katika baraza la madiwani ili kupitisha na kuongeza fedha za malipo ya hapo kwa  hapo. Ndugu Emmanul ameeleza namna fedha za ICHF zikavyowekwa kwenye account itayoandaliwa kwa ajili ya makusanyo kimkoa. Wilaya ya karatu ni moja ya wilaya za mwanzo katika mkoa wa Arusha kuanza kutumia bima ya ICHF.

Ndugu Emmanule muwezeshaji wa semina hiyo amewaasa wasimamizi wa mfuko huo wa bima ya afya iliyoboreshwa ICHF kufanya kazi kwa kujituma. Huduma bora zitawavutia watu wengi kujitokeza na kujiandikisha katika mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa. wawezeshaji hao wametoa vifaa mbalimbali kwa ajili matumizi ya mfumo wa ICHF ambavyo vimepokelewa na Kaimu mganga mkuu wa wilaya ya Karatu.

Dkt. Vicent Gyunda Kaimu Mganga Mkuu amewapongeza wawezeshaji kwa kutoa semina hiyo elekezi kwa wasimamizi wa mfumo wa ICHF. Amewaomba wasimamizi wa ICHF iliyoboreshwa kufanyia kazi kwa vitendo mafunzo waliyopata. Amesema wasimamizi  ni vyema  wakaonesha ueledi katika utendaji wao kwa kuhamasisha wananchi wengi kujiandikisha katika mfuko wa ICHF iliyoboreshwa.

Wasimamizi wakifuatailia semina ka umakini.


Wasimamizi katika matukio mbalimbali kwenye semina.

Wasimamizi katika Matukio mbalimbli wakati wa semina.

Dkt. Vicent akipokea vifaa kwa wawezeshaji wa semina ya ICHF


Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa