• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI KATA WALA KIAPO

Posted on: August 7th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi mkuu  ngazi ya kata unaotarajiwa kufanyika 28/10/2020 wapatao 28 wameapa  mbele ya Hakimu mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Mh. I. Kuppa. Uteuzi wa wasimamizi wasaidizi umeanza rasmi tarehe 5 mwezi wa nane 2020.

Hayo yamesemwa na Msimamizi wa uchaguzi ngazi ya wilaya Ndg. Waziri Mourice wakati akizindua mafunzo ya siku tatu ya wasimamizi wa uchaguzi kwa ngazi ya kata. Ndg. Mourice amesema kila kata itakuwa na wasimamizi wasaidizi wawili.amesema kiapo hicho kinamaanisha wateule hao wamekuwa watumishi wa tume ya taifa ya uchaguzi licha kuwa na majukumu mengine, bado watakuwa wanafanya kazi kama watumishi.

Picha za matukio ofauti wakati wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wakiwa wanaapa

Ndg. Mourice amesema kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata wanatakiwa kutoa taarifa kwa kila jambo wanalolifanya linalohusiana na uchaguzi kwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo au wasimamizi wasaidizi wa jimbo. Ameongeza kusema mambo yote yanayofanywa kuhusiana na uchaguzi hayatolewi ufafanuzi na wasimamizi wasaidizi wa kata, amesema maswala ya uchaguzi yanatolewa taarifa na msimamizi wa uchaguzi wa ngazi ya jimbo au Msimamizi msaidizi wa ngazi ya jimbo au mtu atakayechaguliwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo.

Ndg. Waziri Mourice  Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Karatu akifungua semina ya siku tatu kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata

 Ndg. Waziri Mourice amesema kwa mujibu wakifungu cha 126 cha sheria ya  taifa ya uchaguzi  sura ya 343 tume imepewa mamlaka ya kuandaa  maelekezo mbalimbali kwa ajili ya watendaji wa uchaguzi ili kuwezesha utekelezaji bora wa majukumu yao.  Kwa mujibu wa kifungu cha 7 sehemu ya pili cha sheria ya taifa ya uchaguzi sura 343 kifungu cha tisa sehemu ya pili ya sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa sura ya 292 tume inaweza kuteuwa kwa nyadhifa au kwa majina msimamizi msaidizi wa uchaguzi kwa  jimbo au kata kwa idadi itakayoona inafaa.

Ndg. Mourice amesema sifa kubwa ni kuwa mtumishi wa umma amesema kuna baadhi ya majimbo kwenye nchi yetu wasimamizi wa uchaguzi si wakurugenzi.  Kuwa mkurugenzi wa Halmashauri si sifa pekee kuwa msimamizi wa uchaguzi, amesema tume ya taifa ya uchaguzi imepewa mamlaka ya  kumteuwa mtu yeyeto kwa ngazi ya jimbo au kata. Amesema wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi watatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977; sheria ya taifa ya uchaguzi sura 343 sheria ya gharama za uchaguzi sura 278 kanuni za uchaguzi wa Rais, Wabunge, na Madiwani za mwaka 2020.

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi mkuu  wa ngazi ya wakiapa

Amesema wasimamizi wasaidizi wanatakiwa kufuata muongozo wa utoaji elimu ya mpiga kura na maadili ya uchaguzi ya mwaka 2020 pamoja na maelekezo mengine yatakayotolewa na tume ya taifa ya uchaguzi. Ndg. Mourice amewapongeza walioteuliwa amesema ni vyema wakazingatia mafunzo hayo ya siku tatu yanayofanyika katika ukumbi wa Halmashauri.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa