• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI: AINISHENI NYUMBA ZOTE ZILIZOPO MAENEO YENU

Posted on: February 15th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo amefanya  ziara ya kikazi katika Wilaya ya Karatu leo. Katika ziara yake amekutana na Watendaji wa Halmashauri, Makatibu Tarafa na Watendaji Kata katika ukumbi wa KDA Wilayani Karatu.

Mhe. Gambo amewaelekeza watendaji kusimamia wananchi kulipa kodi ya majengo; amesema watendaji wa kata, watendaji ngazi ya kijiji na kitongoji kutambua idadi ya nyumba zilizopo katika maeneo yao na kuhakikisha nyumba hizo zinalipiwa kodi ya majengo. Kodi ya majengo inalipwa kwa kuangalia hati ya umiliki wa nyumba, na inatakiwa kulipwa kila mwaka. Mwisho wa kulipia kodi hiyo ya majengo kwa mwaka huu ni tarehe 30 Mwezi wa sita.

Mhe. Gambo amewaelekeza watendaji wa kijiji na kata kuja na mpango mkakati kuondoa changamoto ya madarasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na awali katika kipindi cha mwezi wa tatu mpaka wa kumi. Mhe. Gambo amehimiza watendaji kuendelea kufuatilia wazazi ambao wamezembea kupeleka watoto shule, hasa watoto ambao wanapaswa kuandikishwa darasa la kwanza na elimu ya awali. Pia amewaelekeza watendaji kutoa mchanganuo wa wanafunzi 659 waliofaulu kwenda sekondari na hawajaripoti. Lengo likiwa ni kuwawajibisha wazazi walioshindwa kuwapeleka wanafunzi shule kwa sababu za utoro.

Mhe. Gambo amemkabidhi Mkuu wa wilaya ya Karatu viatambulisho vingine elfu kumi na mbili vya wafanyabiashara wadogo. Amesema mtu yeyote atakayekwamisha au kupotosha zoezi hili atakamatwa na kupelekwa mahakamani. Mhe, Gambo amewaelekeza watendaji kuondoa urasimu katika utoaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo.

Awali Halmashauri ya Karatu walipata vitambulisho elfu tatu na sasa wamepata vitambulisho vingine elfu kumi na mbili. Dhamira ya serikali ya kutoa vitambulisho ni kuwaondolea usumbufu ambao wamekuwa wakiupata wafanya biashara wadogo. Mhe. Gambo amesema kitambulisho kinatolewa kwa sekta ambayo siyo rasmi ili wajasiriamali hao waweze kutambuliwa. Serikali inataka wafanyabishara hao wadogo  waweze kukua na kulipa kodi.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa