• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI, ONGEZENI UFUATILIAJI WA TAASISI ZILIZO CHINI YENU

Posted on: May 3rd, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Mazingira mazuri ya kufundisha yanapaswa kutengenezwa na kuwekwa vizuri ili mwanafunzi aweze kusoma katika mazingira rafiki. Ufaulu wa shule za msingi unapaswa kuanzia alama tisini na kuendelea, ni vyema kuongeza uwajibikaji ili kuinua kiwango cha elimu. Walimu wakae karibu na maeneo yao ya vituo vya kazi ili kuongeza ufuatiliaji wa taaluma kwa wanafunzi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea shule ya msingi Marar kukagua miundo mbinu ya elimu. Shule ya Marar ambayo ina  wanafunzi miamoja na themanini na sita na ufaulu wake wa mitihani ya taifa ni alama hamsini. Mh. Kayanda amebaini usimamizi dhaifu wa kiutawala kwa mkuu wa shule, jambo linalochangiwa na mkuu huyo wa shule kuishi mbali na kituo chake cha kazi. Uongozi wa shule kushindwa kuweka mazingira ya shule katika hali ya usafi ili wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri.

Mh. Abbas kayanda akikagua miundo mbinu katika shule ya msingi Marar

 Mh. Kayanda amesema ni vyema walimu wakajiepusha na vitendo vya utoro mahali pakazi jambo ambalo linachangia kuzorotesha elimu. Mwanafunzi ili ajifunze anahitaji ufuatiliaji wa karibu, ameelekeza waratibu wa elimu kata,  kuwa na utaratibu wa kutembelea shule zilizokaribu na maeneo yao kujionea na kujiridhisha na mazingira ya ufundishaji na ufundishwaji ili kuboresha kiwango cha ufaulu wa elimu.

Maelekezo hayo yameenda kwa viongozi wengine kama maafisa tarafa  watendaji kata na watendaji wa wakijiji lengo likiwa ni  kujenga utaratibu wa kutembelea taasisi zinazowazunguka na kuzitambua changamoto zao. Kuzitafutia ufumbuzi na kuwasilisha  kero zilizo nje ya uwezo katika ngazi za juu za maamuzi. Mh. Kayanda amesema hiyo ndio namna nzuri ya kuongeza ufanisi wa kazi kuanzia chini mpaka ngazi za juu.

Katika ziara hiyo Mh. Kayanda ametembelea na kujionea  ujenzi wa matundu vyoo katika shule ya sekondari Kilimatembo na Diego. Amesema lazima ujenzi wa majengo hayo ya vyoo uendane na thamani ya fedha inayotolewa. Shule ya sekondari kilimatembo ujenzi wa matundu kumi ya vyoo, matundu matano kwa ajili ya vyoo vya wavulana na matundu matano mengine ya vyoo kwa ajili ya wasichana. Mh. Kayanda ametoa angalizo kwa watendaji kujiepusha na vitendo vya ubadhilifu wakati wa ujenzi ili thamani ya fedha inayotolewa iendane na thamani ya ujenzi.

Mh. Kayanda ameoneshwa kutoridhishwa na gharama kubwa za ujenzi wa vyoo katika shule ya sekondari ya Diego. Amesema haiwezekani kujengwa matundu kumi ya choo kwa kiasi cha million ishirini na nne mpaka kukamilika. Amesema zipo taasisi ambazo zimefanya ujenzi wa vyoo kwa idadi hiyo hiyo ya matundu kumi ya choo lakini kwa gharama za chini. Ameelekeza kamati ya ujenzi ya shule ya sekondari  Diego kufanya upembuzi upya wa gharama za ujenzi wa maliwato ili kujiridhisha wakati ujenzi wa vyoo ukiwa unaendelea. Lengo likiwa ni kujiepusha na matumizi mabaya ya fedha.

Mh.Abbas Kayanda akiwa katika eneo la ujenzi wa vyoo shule ya sekondari Diego

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa