• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WA KIJIJI NA KATA WAPEWA DIRA YA MAENDELEO

Posted on: August 12th, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Watendaji wa vijiji na kata waaswa kuwa waadilifu na mienendo mizuri katika utendaji wa kazi na kuishi katika maadili utumishi wa umma. Watendaji wa kijiji na kata ndio kioo cha watumishi wa chini mnaowasimamia kwenye ngazi ya kijiji na ngazi ya kata. Lazima mjikite katika kusimamia taarifa za mapato na matumizi na kuhakikisha zinasomwa  kwa wakati ili kujengwa taswira ya uwazi.

Hayo yamejiri katika kikao cha Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda na Watendaji kata na vijiji wote wa wilaya ya Karatu kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri. Amesema kuna watendaji wa vijiji ambao hawajaandika na kusoma taarifa za mapato na matumizi tangu mwaka 2019. Hali hiyo inaleta mashaka katika utendaji wa kazi wa kila siku katika maeneo yao ya kiutawala.

Watendaji wakiwa katika kikao kwenye ukumbi wa Halmashauri

Mh. Kayanda amesema kuna vijiji vinaongoza kwa kuwa na mapato makubwa, lakini hakuna utaratibu wa kukusanya ushuru kwa kutumia (pos) mfumo wa kieletronic. Amesema haya ni mambo ambayo yanapaswa kufanywa na kusimamiwa na watendaji  kama miongozo ya serikali inavyoelekeza.

Mh. Kayanda amesema kuna baadhi ya watendaji wa kijiji hawasikilizi na kufuata maelekezo wanayoelekezwa na watendaji wa kata. Amesema jambo hilo sio sahihi, mtendaji wa kata ni msimamizi wa shughuli zote za serikali katika ngazi ya kata. Mh. Kayanda amekemea tabia nyingine ya watendaji wanaohama kutoka eneo moja kwenda jingine lakini bado anafanya kazi za kituo cha awali bila kukabidhi ofisi, amesema tabia hizo sio nzuri zinaleta usumbufu kwa wananchi wanaohitaji huduma.

picha katika matukio wakati wa kikao cha watendaji wa kijiji na kata

Mh. Kayanda amesema Ofisi za serikali zinapaswa kufanya kazi wakati wote amesema kuna tabia ya za watendaji kutokuwepo katika vituo vya kazi siku za jumamosi na jumapili. Amesema kufanya hivyo kunawanyima wananchi kupata huduma; watendaji wanapaswa kutembelea taasisi zilizo katika maeneo yao  na kujua mwenendo wa taasisi hizo,  pamoja na kutafuta ufumbuzi wa kero na malalamiko ya wananchi katika maeneo yao ya kiutawala.

Mh.Kayanda amesema jukumu la watendaji ni kutoa elimu na kuhamasisha wananchi katika shughuli za kujiletea maendeleo. Amesema watendaji wanapaswa kusimamia kesi za utoro wa wanafunzi shuleni, kusimamia kesi za mimba shuleni ili kudhibiti vitendo hivyo vinavyozorotesha maendeleo ya elimu. Ameongeza kusema mtendaji anapaswa kuhamasisha wananchi juu ya kujiunga na mfuko wa bima ya afya ambayo uandikishaji wake kwa wilaya ya Karatu bado upo chini.  Ameongeza kusema watendaji wanapaswa  kuhamasisha wananchi  juu ya umuhimu wa kuwa na vitambulisho vya ujasiriamali kwa wafanyabiashara wadogo, ambao kwa sasa, Mjasiriamali atalipia  mwenyewe kwenye control number na baadae Afisa biashara wa wilaya  atathibitisha na kutoa kitambulisho.

matukio katika picha wakati wa kikao

Akizungumzia swala la vitambulisho vya mwaka jana Mh. Kayanda amesema kuna kiasi cha million tatu na elfu themanini za mwaka jana ambazo zimepotea kwa njia ya udanganyifu. Ametoa wito kwa watendaji kuhakikisha kiasi hicho cha fedha kinarejeshwa. Kiasi hicho cha fedha  ni malipo ya vitambulisho vya ujasiriamali ambavyo stakabadhi zake zilikaguliwa na mamlaka ya mapato Tanzania (Tra) na kubainika zilikuwa ni stabakadhi feki. Katika malipo hayo ya vitambulisho vya ujasiriamali kuna kata ambazo hazikukutwa na changamoto stakakabadhi feki ambazo ni kata ya Buger,  kata ya Mbulumbulu kata ya Baray na kata ya Endamarariek.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa