• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WA MJI MDOGO WAPEWA DIRA YA MAENDELEO

Posted on: July 13th, 2021



NA TEGEMEO KASTUS

Lazima tuongeze juhudi katika kusimamia ukusanyaji wa mapato ili tuweze kuendelea kujenga miradi ya maendeleo. Kuna wafanyabiashara wanabiashara zaidi ya moja lakini wanaleseni moja ya biashara. Sambamba na leseni lazima tuongeze ufuatiliaji na usimamiaji wa ushuru wa huduma ili tuweze kutimiza malengo tuliojiwekea.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda katika kikao kazi na watendaji wa Mamlaka ya mji mdogo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu. Amesema kuna ulegevu katika ukusanyaji wa mapato kwa watendaji, lazima watendaji wa mamlaka waongeze ubunifu katika kuongeza vyanzo vingine vya mapato ili kuongeza na kuimarisha ukusanyaji wa mapato kama ilivyopitishwa na bajeti ya Halmashauri.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na watendaji wa mji mdogo Karatu. 

Amesema watendaji wa mji mdogo wanapaswa kusimamia usafi wa mazingira katika eneo la mamlaka ya mji mdogo. Hali ya usafi wa mazingira bado hairidhishi, Mh Kayanda amesema watendaji wa mji mdogo waweke mipango mkakati wa kusimamia usafi wa mazingira na kudhibiti tabia za utupaji wa uchafu hovyo, ikiwa ni pamoja na kuweka siku moja kwa ajili ya usafi wa mazingira ili kila mwananchi ajishughulishe na usafi katika eneo lake analoishi.

Watendaji wa mji mdogo katika kikao kazi 

Kuhusu usimamizi wa miradi ya maendeleo Mh. Kayanda amesema watendaji wa mji mdogo  wanapaswa kufuatilia na  kushirikiana na watendaji wa Halmashauri katika kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao. Mh. Kayanda amepongeza jitihada za diwani wa Ganako kwa jitihada zake zakusimamia ujenzi katika zahanati ya Sumawe. Amesema viongozi wa maeneo husika wakifahamu ujenzi wa miradi ya maendeleo inasaidia kujua uhalisia wa mradi wenyewe na inaondoa mianya ya udanganyifu. Ametoa rai kwa viongozi wa mji mdogo kuepuka matumizi mabaya ya madaraka na badala yake waongoze wananchi katika utashi wa kutenda matendo mema.

Akizungumzia hali ya ulinzi na usalama Mh. Kayanda ametoa wito kwa watendaji wa mji mdogo kutoa taarifa za uhalifu kwa vyombo vya ulinzi na usalama. Ameongeza kusema kumekuwa na vitendo vya udokozi katika makazi yetu tunayoishi lakini utoaji wa taarifa za vitendo vya uhalifu umekuwa mdogo. Amesema jukumu la ulinzi na usalama  katika makazi yetu  ni jukumu la kila raia mwema na sio  kwa vyombo vya ulinzi na usalama pekee. Amesema ili kuimarisha ulinzi na usalama ni vyema watendaji wa mji mdogo waanzishe ulinzi shirikishi  katika maeneo ya kiutendaji.

Matukio katika picha wakati wakikao cha watendaji wa mji mdogo na mkuu wa wilaya ya Karatu. 

Kuhusu usikilizaji wa kero za wananchi, Mh, Kayanda amesema watendaji watenge siku moja kwa ajili ya kutatua kero za wananchi. Amesema hakuna jambo la faraja kwa mwanachi kama kiongozi  kusikiliza kero  na kutoa njia sahihi za utatuzi wa chamgamoto zinazomkabili. Amesema changamoto za migogoro ya ardhi ni vyema zikapaelekwa katika baraza la ardhi, changamoto za matunzo ya watoto zipelekwe ustawi wa jamii. Amesema viongozi wanapaswa kuwa wasuluhishi wa migogoro inayotokea kwenye jamii.

Akizungumzia kuhusu swala la kuwa na mamlaka ya mji mdogo kamili mh. Kayanda amesema lazima watendaji wa mji mdogo wafanye tathimini ya vigezo vinavyotakiwa ili waweze kutimiza. Amesema watendaji wa mji mdogo wanapaswa kuwa na mkakati maalumu wa kutimizia vigezo hivyo vya mamlaka ya mji mdogo. Mh. Kayanda amesema anadhamira ya dhati ya kuona siku moja karatu inapata mamlaa kamili ya mji mdogo. Amesema tukipata mamlaka kamili ya mji mdogo kamili itasaidia kuchochea maendeleo ya wilaya ya karatu na itasaidia kupata bajeti mbili katika wilaya moja.

Matukio katika picha wakati wa kikao kazi cha mamlaka ya mji mdogo Karatu. 

kuhusu mafanikio mabalimbali ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, amesema lazima watendaji wazungumze  yaliyotekelezwa katika Halamshauri ya wilaya ya Karatu, Mh Kayanda amesema kua kiasi cha billion 1 ambacho kimetolewa na serikali kupitia wakala wa barabara mjini na vijijini kwa ajili ya kufungua barabara mbalimbali zilizokuwa zimefungwa. Amesema pamoja na kuelezea miradi ya mendeleo iliyofanya na serikali lazima pia tushirikishe wananchi katika usomwaji wa mapato na matumizi katika maeneo yetu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa