• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WATENDAJI WAASWA KUWAJIBIKA KWA BIDII

Posted on: April 30th, 2019

Kikao cha baraza la madiwani kimeendelea kwa siku ya pili leo, na kimejadili taarifa mbalimbali za kamati.  Kikao kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri na kuongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Jublate Mnyenye.

Baraza limejadili taarifa  iliyotoa mapendekezo ya kufidiwa ardhi wananchi waliokuwa wanadai, ili kumaliza baadhi ya migogoro ya ardhi na kuwezesha uendelezaji wa maeneo husika kwa matumizi yaliyopangwa.Wadai sita waliopitishiwa na kukubaliwa na vikao mbalimbali vya Halmashauri kwa ajili ya kufidiwa, ni  Ndugu Benedicto Modaha ambaye kiwanja chake na .67 kitalu ‘k’ Karatu mjini kiliathiriwa na ujenzi / upanuzi wa kituo cha afya Karatu mjini. Ndugu James Paulo kiwanja chake na, 195 kitalu ‘J’ Karatu mjini kiwanja kiligawiwa mara mbili kimakosa. Bi Anastazia Bruno mwenye kiwanja na. 323 kitalu ‘J’ Karatu Mjini kiwanja kiligawiwa mara mbili kimakosa. Ndugu Paskali Sighis mwenye kiwanja  na. 85 kitalu ‘G’ Karatu mjini kiwanja kiliathiriwa na upomaji mwaka 2000 na hakufidiwa. Ndugu Halfa Karonga mwenye kiwanja na.’ G’kambi ya fisi  eneo lake lilipitishwa barabara wakati wa upimaji wa awali wa eneo hilo. Ndugu Baran Akonay mwenye kiwanja na. 137 ‘F’ kiwanja killigawiwa mara mbili kimakosa.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo ametoa maelekezo kwa baraza la madiwani kuchukua hatua kali kwa watendaji waliosababisha wananchi kupewa viwanja mara mbili. Amesema kufanya double allocation ni kosa kubwa sana, ameomba madiwani waiamini kamati ili wanachi wapewe fidia haraka.

Mhe. Theresia ameipongeza Halmashauri ya Karatu kwa kupata hati safi, amesema Halmashauri inaboreka katika utunzaji wa hesabu za serikali. Ameomba watendaji kuondoa hoja za kimfumo ambazo hazitekelezeki. Mhe. Theresia amesikitika kuona wawekezaji waliomba kuwekeza kwenye uwanja wa michezo wa Endoro na chuo cha michezo tangu mwezi wanne mwaka jana lakini wakanyimwa ushirikiano na watendaji. Uwekezaji katika michezo ni fursa ya kiuchumi amehimiza watendaji kushughulikia swala hilo mara moja.

Mhe. Theresia amehimiza baraza  kuongeza mapato ya Halmashauri; amesema kiwanda cha maziwa ambacho kimelala, kinauhitaji wa shilingi million thelathini, ameelekeza baraza la madiwani kuliangalia swala hilo kwa upekee. Kiwanda hicho kikiendelea na uzalishaji kitatoa fursa za ajira, amesema kuna kiwanda cha unga jengo limekamilika tangu mwaka jana. Swala kuendeleza kiwanda cha unga si lazima fedha zitoke  kwenye bajeti ya Halmashauri kama Halmashauri haina uwezo ingie ubia na wawekezaji ili kiwanda kianze uzalishaji.

Waheshimiwa madiwani katika kikao cha baraza la madiwani.

Mhe. Jublate Mnyenye Mwenyekiti wa  Halmashauri akiendesha kikao cha baraza la madiwani.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa