• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WANAOKULA FEDHA MBICHI KIKAANGONI

Posted on: November 8th, 2019

Kikao cha baraza la madiwani kimeendelea kwa siku ya pili mfululizo kwa  kupata taarifa kutoka kamati za Halmashauri. Kikao hicho cha baraza kimeongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Emmanuel Gege.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo ametoa  maelekezo kwa  baraza  kufuatilia ukusanyaji wa mapato vizuri. Amesema amegundua kuna udanaganyifu unafanywa na watumishi wa serikali kwa kutumia fedha wanazotoza  kodi kwa njia ya point of sales (POS)  na kuzitumia fedha hizo kinyume na utaratibu. Mhe. Theresia amesema ameshampa maelekezo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karatu kufuatilia na kuchukua hatua kali dhidi ya watendaji waliohusika. Amesema fedha za ukusanyaji wa mapato zinasaidia katika shughuli za maendeleo, kumalizia miradi viporo na kulipa madai ya watumishi.

Mhe. Theresia amesema kuna udhaifu pia wa kiutendaji katika kitengo cha manunuzi cha Halmashauri ya wilaya ya Karatu. Amesema kitengo hicho hakifuati sheria za manunuzi, Mhe. Theresia amesema amebaini hayo baada ya kuunda tume kuchunguza ujenzi wa hospital ya wilaya. Katika taarifa yake kamati ilibaini kuna vifaa vilinunuliwa na havikufika eneo la ujenzi lakini vimeshalipiwa, amesema kuna dawa zimenunuliwa kuzidi mahitaji za kunyunyiza wadudu ili kuzuia uharibifu wa mchwa. Lakin kuna kokoto zilizozidi mahitaji, rola zimenunuliwa nyingi kuzidi mahitaji, ameliagiza baraza kupitia kamati ya fedha kutimiza wajibu wao kukagua miradi. Mhe Theresia amesema amekabidhi TAKUKURU wilaya karatu taarifa hiyo ya uchunguzi wa ujenzi wa hospitali kwa ajili kuchukua hatua zaidi za kisheria.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Emannuel Gege akiongoza  kikao cha baraza la madiwani

Ndugu waziri Mourice Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Karatu, amesema watu wanazitumia fedha za mapato ambazo zinapaswa kuwekwa benk. Ndugu Mourice amesema tayari ameshakamata baadhi ya watu na kuwaweka ndani kutokana na kutumia fedha za makusanyo ya mapato ya serikali kinyume na utaratibu. 

Ndugu Waziri Mourice amesema amemuandikia Mtunza Hazina kwa maandishi akimuelekeza umuhimu wa kusimamia ukusanyaji wa  mapato vizuri na pia kusimamia matumizi mazuri ya fedha. Ndugu Mourice amesema Halmashauri iko mbioni kufunga mfumo wa mapato ofisi ya mkuu wa Wilaya ili kusaidia kuona mwenendo wa ukusanyaji wa kodi wa Halmashauri.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa