• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI: KUMNYIMA MTOTO CHAKULA KUNASABABISHA UDUMAVU

Posted on: June 17th, 2019

Mama akiwa anafurahia mtoto wake katika sherehe ya siku ya mtoto wa Afrika

Maadhimisho yasiku ya mtoto wa Afrika ngazi ya wilaya yamefanyika katika Tarafa ya Endabash. Sherehe hizo zimeenda sambamba na uzinduzi wa chanjo ya vitamin A kwa watoto wadogo. Mgeni rasmi katika sherehe ya siku ya mtoto wa Afrika alikuwa mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo.

Mhe. Theresia amelipongeza shirika la World vision kwa ujenzi wa miundo mbinu yaa madarasa maji na afya. Mhe. Theresia amesema Way-Bantwana na Shidepa wametekeleza mradi wa waache wasome  ambao unaenda vizuri na wameandaa vikundi vya kuinua uchumi wa wananchi vinavyoshirikisha wanawake na wakinababa wachache. Mhe. Theresia amewapongeza shirika la Compassion kwa kuwalipia ada na kuwaendeleza watoto  katika mafunzo ya Tehama pia amewapongeza pia vituo vinane vya kulea watoto.

Mhe. Theresia Mahongo amewapongeza wadau kwa kupunguza tatizo la mimba shuleni. Amesema mwaka jana kulikuwa na mimba 15 shule ya msingi na sekondari 25. Mwaka huu kuna taarifa 2 za mimba kwa shule ya msingi na sekondari hakuna hili ni tatizo kubwa. Mhe. Theresia amesema swala la ajira za watoto limeendelea kuwa changamoto Tarafa ya Eyasi. Amewaomba wazazi kulionea haya jambo hilo imekuwa mtoto ndiye anayelea mzazi badala ya mzazi kumlea mtoto. Mhe. Theresia amemuagiza katibu Tarafa wa Eyasi kupambana na ajira za watoto katika mashamba ya vitungu kwa kuwakamata wazazi wanaojihusisha na kuwaachia watoto kwenda kufanya kazi kwenye mashamba ya vitunguu ili kujipatia ujira.


Mhe. Theresia amesema wazazi wamerudi nyuma katika kujitolea kuwapatia chakula watoto wanapokuwa shuleni. Amesema tarafa ya Endabash imerudi nyuma katika swala la kuwapatia watoto chakula shuleni. Amesema ni shule moja ya Raja inayotoa chakula cha mchana kwa watoto, amesema unapomnyima mtoto chakula unamsababishia udumavu. Mtoto anashindwa kufanya vizuri shuleni kutokana na kukosa chakula. Kuna sheria na 21 ya mtoto ya  mwaka 2009 na kanuni za mtoto. Sheria hii inaonesha mzazi ambaye hamtunzi mtoto apewe adhabu zinazo  muwajibisha. Amesema kauli mbiu inasema “mtoto ni msingi wa taifa endelevu, tumtunze, tumlinde na kumuendeleza” Mhe. Theresia amesema hata sita kumchukulia hatua mzazi yeyote ambaye anashindwa kumhudumia mtoto kwa kumpatia chakula anapokuwa shuleni. Amesema watoto wanavipaji mbalimbali, wazazi  tunapaswa kulea watoto ili watimize ndoto zao.

Mhe. Theresia amewaasa wanachi kuhifadhi chakula amesema kuna maeneo kama ya kata ya Mbulumbulu na Mang’ola wamepata chakula. Amesema maeneo ya Endabash mpaka Baray Khusumay na kule Rhotia  mazao hawakupata vizuri ni vyema kuhifadhi na kununua akiba ya chakula.

Mhe. Theresia amesema kuna uchaguzi wa serikali za mitaa, amewaomba wanachi kujitokeza kupiga kura. Amesema ni vyema wananchi wakajiepusha na vitendo vya rushwa nyakati za uchaguzi. Amesema ni vyema wananchi wakachagua viongozi  bora, ambao watakuwa chachu ya maendeleo.

Mhe. Theresia ametoa taarifa kwa wananchi juu ya kuwepo kwa kikao cha wafanyabishara  kitakachofanyika tarehe 20 mwezi huu. Ameomba wafanyabishara wote kujitokeza ili waweze kusema changamoto zao zinazowakabili katika shughuli zao za kibiashara. Kikao hicho kitajumuisha wafanyabishara kutoka sehemu mbalimbali za wilaya ya Karatu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa