• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WADAU WAASWA KUSIMAMIA HAKI ZA WATOTO

Posted on: February 22nd, 2019

Shirika la kikristo la Compassion limefanya semina ya siku tatu juu ya namna kumlinda mtoto juu ya unyanyasaji. Semina hiyo iliyoisha jana katika kanisa la T.A.G Karatu imehusisha wadau wanaojihusisha na malezi ya watoto.

Ndugu Lameck Karanga Afisa Tarafa wa Karatu amefunga semina hiyo na amesema ni vyema semina za ufahamu wa namna ya kuwalinda watoto, wakapewa pia wazazi na jamii. Amesema semina kama hizo zinaweza zikafanywa shuleni, ambayo ni sehemu raisi ya kupata watoto. Amesema serikali itahamasisha kupitia mikutano ya umma ili wazazi na jamii iweze kupata ufahamu. Ndugu Lameck amesema kinga ni bora kuliko madhara yanayoweza kujitokeza baadae.

Bi, Elizabeth Madata, Afisa Ustawi wa jamii amesema semina hiyo imewasaidia kujifunza hatua za ukuaji wa mtoto. Maamuzi ya kuchukua pindi mtoto anapoathirika na unyanyasaji wa kijinsia lakini pia sehemu ya kuripoti pindi tattizo linapotokea. Bi Elizabeth amesema mtoto (infanty) anatakiwa awe karibu na wazazi wake hasa mama ili aweze ( Kujenga trust ) kuamini wazazi. Mzazi anatakiwa kumfutilia mtoto kwa karibu katika ukuaji wake ili aweze kujua kipaji chake.

Bi Elizabeth amesema changamoto walizokuwa wanazipata awali juu matukio ya unyanyasaji watoto ni mawasiliano duni kati ya wadau na vyombo vya serikali. Amesema kupitia semina hiyo imekutanisha wadau wote husika na imewasaidia kufahamiana lakini pia namna ya kuunganisha nguvu zao kwa pamoja dhidi ya unyanyasaji wa watoto. Amesema semina hiyo imewasaidia wadau kufahamu sehemu za kuripoti pindi matukio ya unyanyasaji yanapotokea.  Amesema  kuna hofu ya kutoa taarifa kwenye tukio la ukatili wa kijinsia kwa kuogopa uhasama, semina hiyo imewajengea uelewa mkubwa wadau.

Bw. Amani Lohay ambaye ni mdau amesema kwao katika semina hiyo, shirika la compassion limewapa njia  nne za kuhudumia watoto amabazo ni kimwili kwa kumpa chakula na mazoezi. Lakini pia mtoto anajengwa kiroho kwa kupata mafundisho ya kiimani, na kiakili kwa mtoto kupewa akili ya ujasiriamali na ubunifu. Watoto wanajengewa namna njema ya kuhusiana na jamii na kuishi maisha  yanayofaa.

Naye Mchungaji Samweli Kibola amesema mtoto wamekuwa wakinyanyaswa na  kumekuwa  hakuna mtetezi. Jamii imekuwa na mwamko duni wa kutetea haki za watoto, semina hiyo imesaidia mbinu za kumlinda mtoto. Amehimiza wazazi kutambua wajibu wao na kutimiza majukumu ya kumlinda mtoto

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa