• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAZIRI, ATOA MILLION 300 KUJENGA MIRADI YA MAJI KARATU

Posted on: March 5th, 2020

Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa amefanya ziara ya siku moja wilaya ya karatu. Amekagaua miradi ya maji katika tarafa ya Karatu mjini na tarafa ya Endabash na kupokea taarifa ya miradi ya maji ya wilaya.

Waziri wa maji ametoa kiasi cha Million 300  kwa kuanzia kwa ajili ya undelezaji wa miradi ya maji wilayani Karatu. Miradi ya maji ambayo itaanza kufanyiwa kazi kutokana na fedha hizo ni mradi wa maji Ayalabe kata ya Ganako; mradi wa maji bwawani kata ya Karatu, mradi wa maji Kansay  kata ya Kansay na Mradi wa Maji Buger kata ya Burger. Amesema watatumia force account katika utekelazaji wa miradi hiyo na vifaa vitanunuliwa kwa pamoja ili kupunguza gharama za manunuzi. Mhe. Waziri wa Maji  Profesa Mbarawa amesema watajikita katika ununuzi wa mabomba, watajikita katika ununuzi wa pampu za maji na kuanza kutoa fedha kidogo kwa ajili ya ujenzi wa matanki  ya maji mawili.

Mhe. Waziri wa Maji  Profesa Mbarawa ametembelea mradi wa kwa Tom ulipo karatu Mjini. Katika mradi huo Mhe. Waziri Profesa Mbarawa amesema upatikanaji wa maji upo chini sana wilayani karatu. Gharama za mradi wa maji kwa Tom ni takribani million 500 na gharama zilizobakia ili kukamilisha mradi ni million 209. Mhe. Waziri ameahidi kutoa fedha za mradi huo zilizobaki mwezi huu, ili kuhakikisha mradi umemalizika kwa 100% kwa sasa mradi ujenzi wake umefika 75%. Amesema mradi huo ukimalizika upatikanaji wa maji katika mji wa Karatu utafikia 52%.

Katika kikao cha ndani Mhe. Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Mbarawa amesema miradi ya maji kwa kipindi kirefu haikufanywa kwa viwango vinavyostahili. Amesema sisi wote hatukuwafanyia wananchi haki, ndio maana tumeanzisha RUWASA na kuhakikisha miradi yote ya maji inatekelezwa. Profesa Mbarawa amesema jambo la pili ni kuhakikisha wakandarasi wa hovyo tunaachana nao na kazi zinafanywa na wataalamu wa RUWASA. Profesa Mbarawa amesema mpaka sasa hakuna kibali kilichotolewa kwa mkandarasi yeyote wizarani.  Hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa dhidi ya wakandarasi wazembe, Profesa Mbarawa amesema jambo la kwanza kwa sasa kwa watanzania ni kuhakikisha tunaleta maji safi na salama.

Profesa. Makame Mbarawa (kulia) akikagua mradi wa maji kwa Tom, Karatu Mjini.

Naye Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya maji. Mhe. Mahongo amemshukuru pia Waziri wa Maji  Profesa Makame Mbarawa kwa kuja kuona changamoto ya maji wilayani Karatu. Amesema miradi minne ambayo fedha inakuja mwezi huu, itasimamiwa na watendaji wa maji badala ya wakandarasi wa maji hivyo miradi itatekelezwa haraka mpaka mwezi wa saba mwaka huu huduma za maji zitaanza kupatikana. Mhe. Mahongo amememuahidi Waziri wa Maji  Profesa Mbarawa, kwamba yeye pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama watailinda miundo mbinu ya maji. Mhe. Mahongo ametoa wito kwa wananchi  kuendelea kutunza miundo mbinu ya maji.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Karatu; Ndugu Waziri Mourice amesema, maeneo vilipochimbwa visima vya Ayalabe  yalikuwa ni maeneo ya watu. Wenye maeneo waliridhia kabla zoezi la uchimbaji wa maji, tayari wataalamu walishaenda kupima kuona ni eneo gani wataweka mipaka kwa ajili ya maji na eneo gani wananchi wataendalea kulitumia kwa ajili ya shughuli zao. Ndugu Mourice amemuhakikishia Mhe. Waziri Profesa Mbarawa eneo hilo halina tatizo. 

Mhe Willy Qambalo, ameeleza kilio cha wananchi wa kata ya Kansay ambele ya Waziri wa Maji Professa Mbarawa kwamba wananchi hawaamini viongozi wao hasa wanapozungumzia kuhusu Maji.  Ameongeza kusema mradi wa maji wa Kansay wamekuja viongozi wengi lakini bado tatizo limeendelea kuwa sugu, amesema kutokana na adha ya maji wananchi wa Kansay wanalazimika kwenda kutafuta maji katika maeneo ya Hifadhi za wanyamapori jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa maisha yao.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa