• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WENYEVITI WA VITONGOJI; ANZISHENI ULINZI SHIRIKISHI

Posted on: July 13th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo amefanya mkutano na wananchi wa Karatu katika uwanja wa mazingira bora. Ametumia mkutano huo pia kusikiliza kero mbalimbali za wananchi wa wilaya ya Karatu walizo mueleza.

Mhe. Theresia amesema Karatu mjini kuna vibaka sana jambo linalo hatarisha usalama wa wananchi na mali zao. Amesema vibaka hao wengi ni vijana, amesema kama inafikia mahali huwezi ukaweka nguo nje zimepitiwa huwezi ukafuga kuku watu wameiba inaumiza sana. Amesema Karatu tunategemea utalii sana, kuna watu wanapita kwenda mbugani ndio maana tunafanya biashara. Amesema hatuwezi kuwa na taifa la wezi na vibaka, amekumbusha na kusisitiza wafanya biashara kufunga kamera za ulinzi kwenye biashara. Ameelekeza wenyeviti wa vitongoji kuanza ulinzi shirikishi ili kukabiliana na uhalifu wa wizi unaoendelea na kuhatarisha hali ya usalama wa watu na mali zao.

Mhe. Theresia amesema kama Mkuu wa wilaya jukumu lake ni kusimamia ulinzi masaa 24, amewaasa  wananchi juu ya kupanda mshikaki.amesema kwenye mtandao kuna matukio mengi ya watu kuvamiwa na kunyang’anywa pikipiki zao hasa nyakati za usiku. Amewaasa wananchi kuchukua tahadhari hasa nyakati za usiku kwa kupanda pikipiki kwa mtu unayemfahamu.

 Amezungumzia pia swala la madereva bodaboda, amesema kwenye kikao walichokaa waendesha bodaboda walikubaliana muda wa mwisho wa kufanya kazi ni saa sita usiku. Amesema kuna vituo viwili ambavyo vina leseni ya kufanya biashara usiku kucha, hapo bodaboda walikubalina katika vituo hivyo viwili kuwepo na kufanya shughuli zao. Hivyo hata wakikutwa na watu wa ulinzi shirikishi watajitambulisha na wataendelea na kazi zao.

Wananchi wakifuatilia mkutano katika uwanja wa mazingira Bora

Mhe. Theresia amesema muda wa mwisho wa kufunga baa kwa siku za kazi ni saa tano usiku na hufunguliwa saa kumi alasiri baada ya mida ya kazi. Amesema kwa siku za sikukuu au mwishoni mwa juma baa hufunguliwa saa kumi na kufungwa saa sita usiku.

Mhe. Theresia amewaasa wananchi kuacha mila potofu za kuficha uovu, amesema  watu wanao fanya uovu wanafahamika. Nivyema wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi, ili wakamatwe na hatua kali dhidi yao zichukuliwe. Kumekuwa na tabia za wananchi kuficha wahalifu hasa kwa wale watu wanaobaka mabinti.  Amesema tabia hizi zinakatisha ndoto za wasichana kufikia malengo yao. Amewaomba wananchi kutoa ushirikiano  kubaini wahalifu na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. Haiwezekani watu wafanye uhalifu halafu wanakubaliana kusuluhisha kwa kupeana madume ya ng’ombe.

Awali wananchi katika kikao hicho walimueleza mkuu wa wilaya kero zinazowasumbua, ndugu Onesmo Tarimo amemueleza mkuu wa wilaya kwamba kuna kesi za ubakaji nyingi ambazo jamii inazifumbia macho. Hakuna hatua za kisheria zinazochukuliwa juu yao baada ya wananchi kushindwa kutoa ushirikiano kwa polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe juu yao.

Naye Mwenyekiti wa kitongoji cha Bwawani Ndugu Joshua Nangay amemueleza kero wanazopata juu ya utofauti wa muda kufunga baa. Amesema kuna baadhi ya baa ni mali ya wafanyakazi na ni marafiki na jeshi la polisi, baa zao hazifungwi ila hizi za watu wengine zinafungwa mapema. Wezi na vibaka hukaa kwenye baa hizo wakati wakivizia kufanya uhalifu usiku, hivyo kumuomba mkuu wa wilaya kutoa maelekezo juu ya jambo hilo.

wanachi wakifuatilia mkutano kwa makini

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa