• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WENYEVITI WAASWA KUSIMAMIA SHUGHULI ZA MAENDELEO

Posted on: December 3rd, 2019

Wenyeviti wa kijiji na vitongoji waliochaguliwa na kupita bila kupinga kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wameapishwa. Zoezi la uapishaji viongozi hao limefanyika kwa muda wa siku mbili, ili waanze kutekeleza majukumu yao ya kazi.

Msimamizi wa uchaguzi wilayani Karatu Ndugu Pius Haule amesema uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika ulifuata kanuni na miongozo iliyoweka. Amesema kutofuata kanuni hizo kulisababisha wagombea wengi kushindwa kutimiza mahitaji ya ujazajaji wa fomu. Amesema ilikuwa ni jukumu la vyama vyote vitano vilivyopewa kanuni na miongozo ya uchaguzi wa serikali za mitaa kufuata maelekezo kikamilifu. Dosari ndogo za ujazaji wa fomu ndizo zilizoengua wagombea wengi na kusababisha kukosa sifa wakati wa uchaguzi. Amesema vyama vya siasa vilipaswa kutoa elimu hiyo kwa wagombea wao ili kuepuka dosari zilizojitokeza.

NDUGU PIUS HAULE AKITOA MAELEKEZO WAKATI WA UJAZAJI WA FOMU ZA KIAPO

Ndugu Pius Haule amewaasa viongozi walioapishwa kuepuka migorogoro ya uongozi katika utendaji wa shughuli zao sehemu za kazi. Amesema isitokee Mwenyekiti wa kijiji anagombana na Mtendaji wa kijiji katika utekelezaji wao wa shughuli za serikali. Amewaomba watendaji wa vijiji kusimamia ukusanayaji wa mapato katika maeneo yao ili waweze kutekeleza miradi ya maendeleo.

Ndugu Haule amewaasa viongozi hao kujiepusha na vitendo vya rushwa katika kipindi chao cha uongozi. Kuna tatizo moja kati ya watendaji wa vijiji na wenyeviti wa kijiji katika ukusanyaji wa mapato. Amesema mtendaji wa kijiji ni Afisa mhasibu wa kijiji, yeye ndiye anakusanya fedha na atafanya matumizi ya kijiji kwa ridhaa ya uongozi wa kijiji. Amesema wenyeviti wa vijiji ni wasimamizi wa vijiji wanahakikisha mapato na matumizi ya kijiji yanasomwa kila robo ya mwaka. Amesema Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Karatu ataandaa semina elekezi kwa wenyeviti  ili kuwaelimisha mipaka yao ya uongozi katika kufanya kazi kwa pamoja na watendaji wa vijiji.

Hakimu mfawidhi wa wilaya Mhe. I.B Kuppa amesema ukila kiapo kwa kamishina wa kiapo kama Hakimu au wakili yeyote unajipa jukumu. Kiapo kinatoa nafasi kwa kiongozi yeyote aliyekula kiapo kuchukuliwa hatua za kisheria kama ataenda kinyume na masharti ya kiapo.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha kambi ya Simba ndugu Faustine Simon Lulu ambaye  awali alikuwa mwenyekiti wa kitongoji, amesema atafuata utaratibu wa kisheria na kanuni za uendeshaji wa kijiji kwa kuunda kamati za kudumu ili kusiamamia maendeleo ya kijiji. Amesema kwa kushirikiana na Halmashauri ya kijiji wataongoza shughuli za uzalishaji, na atawatumikia wananchi na wanakijiji wa Kambi ya simba kwa misingi ya utawala bora. Ikumbukwe kwamba nafasi zote za wenyeviti zimechukuliwa na chama cha mapinduzi kwa kushinda sehemu zilizofanya uchaguzi na wagombea wake kupita bila kupigwa kwa maeneo ambayo hawakufanya uchaguzi.

WENYEVITI WAKIWA WAMENYANYUA MIKONO JUU IKIWA NI ISHARA YA KULA KIAPO MBELE KAMISHINA WA KIAPO

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa